| Wapendwa kaka na dada zangu,
1. Katika Jumapili ya Umisioni duniani, mwaka huu umetolewa ujumbe
(Kaulimbiu) wa Ekaristi, unatusaidia kujua vizuri zaidi umaana wa
Ekaristi katika maisha yetu, wakati tunaendelea kuishi dhamira ya
Chumba cha Juu wakati katika undani wa mateso yake, Yesu alijitoa
mwenyewe kwa Ulimwengu: “Usiku ule alipotolewa, alichukua
mkate, na baada ya kushukuru, aliumega na kusema: huu ndio mwili
wangu unaotolewa kwa ajili ya yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka:
(1Kor. 11:23-24).
Katika barua yangu ya kichungaji ya hivi karibuni ‘Mane nobiscum
Domine’, niliwaalika kutafakari juu ya Yesu katika “Kuumega
Mkate” uliotolewa kwa ajili ya binadamu wote. Kwa kufuata
mfano wake sisi nasi tunaitwa kuyatoa maisha yetu kwa ajili ya ndugu
zetu na hasa wale wanaohitaji msaada wetu. Ekaristi ni “Ishara
ya Umoja duniani” na kwa muono wa kisakramenti inaonyesha
jinsi, “wote wanaoshiriki hali moja ya kibinadamu, waliozaliwa
katika Kristo kwa njia ya Roho Mtakatifu na wanatwaa Utukufu wa
Mungu, watakavyoweza kusema kwa pamoja: “Baba Yetu”
(Ad Gentes 7). Kwa njia hii, wakati Ekaristi inasaidia kuelewa kikamilifu
zaidi maana halisi ya MISIONI, inamwongoza kila muamini, kwa namna
ya peke kila mmisionari, ili awe “Mkate, uliomegwa kwa ajili
ya uhai wa dunia.”
2. UBINADAMU UNAMUHITAJI KRISTO “MKATE ULIOMEGWA”
Katika maisha yetu ya kila siku jamii ya kibinadamu inaonekana
imefunikwa na dimbwi la vivuli vya giza wakati inatikiswa na matukio
mazito yanayoleta uharibifu mkubwa wa mazingira katika dunia. Hata
hivi kama vile “Usiku ule alipotolewa (1Kor. 11:23)”
hata leo Yesu, “Anaumega Mkate.” (e.g. Mt. 26:26) kwa
ajili yetu katika Ibada ya Ekaristi na anajitoa sadaka katika alama
ya Sakramenti ya upendo wake kwa binadamu. Ndiyo maana nilieleza
kwa msisitizo kwamba “Ekaristi si tu ni Ishara ya Umoja katika
maisha ya kanisa, bali pia ni mfumo wa mshikamano wa wanadamu wote.”
(Mane nobiscum Domine, 27; ni “Mkate kutoka Mbinguni”
unaoleta uzima wa milele (cf. Jn. 6:33) na unauelekeza moyo wa mwanadamu
kwenye tumaini kubwa zaidi.
Akiwa katika Ekaristia, Mkombozi yule yule aliyeona uhitaji wa
kundi na akajaa moyo wa huruma “Kwa vile walikuwa wanateswa
na kutupwa, kama kondoo wasio na mchungaji,” (Mt. 9:36) anaendelea
katika karne (nyakati) kuonyesha upendo wa binadamu maskini na walio
katika mateso.
Na ni katika jina lake ambapo wachungaji na wamisionari wanaeendelea
kwenda sehemu ambazo bado hazijulikani kupeleka “Mkate”
wa wokovu kwa wote. Wanasukumwa na ufahamu kuwa, muungano na Kristo
“kiini si tu cha historia ya kanisa, bali pia cha historia
ya ubinadamu (Ef. 1:10, Cal.1:15-20)” Mane naobisum Domine
6), inawezekana kuona kwa undani kabisa kiini cha moyo wa binadamu.
Yesu pekee ndiye anaweza kutosheleza mahitaji ya njaa ya Upendo
na kiu ya Haki katika binadamu; ni yeye pekee anamfanya mwanadamu
ashiriki katika maisha ya umilele: “Mimi ni mkate wa uzima
ulioshuka duniani kutoka Mbinguni. Yeyote aulaye mkate huu ataishi
milele” (Jn. 6:51)
3. KANISA, LILILO MOJA PAMOJA NA KRISTO, LINAKUWA “MKATE
ULIOMEGWA”.
Wakati jumuiya ya Kanisa inaadhimisha Ekaristi na hasa Jumaipili,
Siku ya Bwana, inagusa katika mwanga wa imani, thamani ya kukutana
na Kirsto Mfufuka na kwa namna ya pekee inaelewa zaidi kwamba Sadaka
ya Ekaristi ni kwa ajili ya wote (Mt. 26:28). Na sisi tunaoshiriki
katika Mwili na Damu ya Bwana aliyesulibiwa na Kufufuka, hatuwezi
kuiweka zawadi hii iwe kwa ajili yetu tu; kinyume chake, ni lazima
tushirikishe. Upendo wa kisadaka kwa Kristo unatuongoza kumtangaza
Kristo kwa ushujaa; ambapo kumtangaza huko katika ushahidi unakuwa
ni sadaka kuu ya upeo katika kumpenda Mungu na Binadamu.
Ekaristi inatuongoza tuwe wainjilishaji wakarimu, wenye kujitoa
kikamilifu katika kujenga ulimwengu wenye haki na udugu zaidi.
Kwa hakika natumaini mwaka wa Ekaristi utaiangaza kila jumuiya
ya Kikristo kutoa jibu lenye “Mwamko wa Udugu katika baadhi
ya namna nyingi za umaskini uliopo katika dunia yetu.” (Mane
nobiscum Domine 28), kwa sababu “Kwa kupendana kwetu na kwa
namna ya pekee kwa kuwajali zaidi wale walio katika shida zaidi,
tutajulikana kuwa wafuasi kweli wa Kristo (Yoh. 13:35; Mt.25:31-46).
Hiki kitakuwa ndicho kipimo cha kuhukumu ukanuni wetu katika kuadhimisha
ibada zetu za Ekaristi.” (mane nobiscum Domine 28).
4. WAMISIONARI, “MKATE ULIOMEGWA” KWA AJILI
YA UHAI WA ULIMWENGU.
Bado hata leo Kristo anawaambia wanafunzi wake: “Wapeni chochote
cha kula ninyi wenyewe” (Mt. 14:16). Kwa jina lake wamisionari
duniani kote wanatangaza na kushuhudia Injili. Kwa njia ya juhudi
zao yanasikika tena maneno ya Mkombozi: “Mimi ni chakula cha
Uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa; naye aniaminiye hataona
kiu kamwe.” (Yoh. 6:35) nao wanakuwa pia “Mkate uliomegwa”
kwa ajili ya ndugu zao, na wengine hadi kufikia kuutoa uhai wao.
Ni wamisoonari wangapi mashahidi katika nyakati zetu hizi! Tunatakia
mfano huo uwaite vijana wengi wa kike na kiume kuthubutu kufuata
njia ya ushujaa wa kiimani kwa Kristo! Kanisa linahitaji watu wake
kwa waume kujitoa wakfu kikamilifu kwa ajili ya kuifuata njia kuu
ya Injili.
JUMAPILI YA MISIONI ni wakati mwafaka wa kuongeza uelewo wetu juu
ya umuhimu wa haraka wa kushiriki katika Utume wa Uinjilishaji katika
jumuiya zetu na katika taasisi nyingi za kanisa na hasa vyama vya
Kipapa vya Kimisionari na katika mashirika ya kimisionari.
Umisionari huu unahitaji msaada si tu wa Sala na sadaka, bali pia
msaada wa mahitaji kamili. Natumia fursa hii kuwakumbusha bado juu
ya uthamani na umuhimu wa huduma inayotolewa na Vyama vya Kipapa
vya Kimisionari na nawaombeni nyote kuyachangia kwa ukarimu wote
katika ushirikiano wa Kiroho na Kimahitaji.
Bikira Maria, Mama wa Mungu atusaidie kupunguza uzito wa Chumba
cha Juu ili kwamba Jumuiya zetu za Kanisa ziwe za “Kikatoliki”
zaidi, yaani ziwe jumuiya ambako “roho ya kimisionari”
iliyoshikamana kwa undani na Kristo (Rm. 88), iwe karibu katika
uhusiano wake katika “roho ya Ki-Ekaristi” ambapo Bikira
Maria ni mfano, “Mwanamke wa Ekaristi.” (Ecclesia de
Eucharistia 53); Jumuiya ambazo daima zipo tayari kwa kusikia sauti
ya Roho na kwa mahitaji ya Ubinadamu, jumuiya ambapo waamini, na
hasa wamisionari hawasiti kujitoa wao wenyewe kama, “Mkate,
iliomegwa kwa ajili ya uhai wa Ulimwengu.”
Kwa wote natoa Baraka ya kichungaji.
Kutoka Vaticani, 22 February 2005, Sikukuu ya Ukulu wa Petro.
Yohane Paulo II |